Top Ad unit 728 × 90

.

Chidi Benz kufikishwa mahakamani Leo.


Rapper Chidi Benz anatarajiwa kufikishwa mahakamani siku ya leo kujibu mashitaka kutokana na kesi ya kukamatwa na Dawa za Kulevya, tukio lililotokea Ijumaa wiki iliyopita.

Kwa mujibu wa Kamanda Geofrey Nzowa, Mkuu wa Kikosi cha kupambana na dawa za Kulevya nchini, Chidi Benz atafikishwa katika mahakama ya Kisutu ambapo atasomewa mashitaka yake kwa mara ya kwanza.

Chidi alipatikana na dawa za kulevya aina ya Heroine kete zipatazo 14 pamoja na misokoto ya Bangi katika kiwanja cha ndege cha Julius Nyerere akiwa anaelekea Mbeya kwa shughuli za kimuziki.
Sammisago.com ndio mtandao wako kwa habari za burudani Africa na nje, Tuwe pamoja huku pia >> Instagram , Twitter Na Facebook

Chidi Benz kufikishwa mahakamani Leo. Reviewed by Unknown on Tuesday, October 28, 2014 Rating: 5
All Rights Reserved by SamMisago.Com © 2014 - 2015
WebDesigned by iDodo enterprises

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.